Wahariri Waipongeza REA — Gesi Asilia Lindi & Pwani

Xmation Media
By -
0
Wahariri Waipongeza REA — Gesi Asilia Lindi & Pwani | XNEWS CHANNEL
Jumanne, 8 Machi 2026 · Dar es Salaam, Tanzania
Xmation Media
LIVE
HABARI
Wahariri TEF waipongeza REA Bilioni 6 kwa kaya 1000 — Gesi Asilia Lindi & Pwani Mradi wa 100% Fedha za Serikali kupitia REA Mwenyekiti Balile: "REA imefanya kazi kubwa sana" TPDC Mha. Karomba awasihi wananchi kuilinda miundombinu Wananchi wa Kisemvule wanashukuru Serikali
Nishati · Pwani & Lindi

WAHARIRI WAIPONGEZA REA USAMBAZAJI WA GESI ASILIA LINDI, PWANI

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limetoa pongezi kwa Serikali kupitia REA kwa mradi wa kusambaza gesi asilia unaonufaisha kaya 1,000 na shule moja — ukifadhiliwa na Serikali kwa asilimia 100.

1,000
Kaya Zilizounganishwa
Mkoa wa Lindi & Pwani
Bil. 6
Shilingi za Mradi
Fedha za Serikali
100%
Ufadhili wa Serikali
Kupitia REA / REF
1
Shule Iliyounganishwa
Kata ya Kisemvule
IE
Iyan Eman
Published by · XNEWS Channel
8 Machi 2026
Dakika 5 kusoma
Dar es Salaam, Tanzania
💰
Bilioni 6 yawezesha kusambaza miundombinu ya gesi asilia kwenye kaya 1000 na shule moja
Nishati ya gesi asilia ni ya uhakika, salama na nafuu zaidi kuliko nishati nyingine
🛡️
Wananchi watakiwa kuilinda miundombinu ya kusambaza gesi asilia

"REA imefanya kazi kubwa sana ya kufadhili mradi huu, hivyo basi mradi huu utaboresha kiwango cha maisha ya walengwa wa mradi kwa kuokoa gharama na muda wa kupika, mazingira safi afya bora na uwezeshaji wa wanawake kuongezeka."

Bw. Deodatus Balile — Mwenyekiti, Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kusambaza miundombinu ya gesi asilia kwenye kaya takribani 1000 na shule moja ambapo mradi huo umefadhiliwa na Serikali kwa asilimia 100 kupitia REA.

Hayo yamezungumzwa leo Machi 8, 2026 na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Bw. Deodatus Balile wakati wa Ziara ya TEF Kutembelea mradi uliofadhiliwa na REA wa ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa gesi asilia kwenye nyumba za makazi mkoa wa Pwani.

Bw. Balile amesema kupitia mradi huo Serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa Nishati nyingine kama mkaa wa kawaida, kuni, na mafuta ya taa na nishati gesi asilia sasa inakua ni chanzo cha nishati ya kupikia.

Nishati Safi & Salama
Gesi asilia ni salama, nafuu na ya uhakika zaidi kuliko mkaa, kuni na mafuta ya taa.
🌿
Kulinda Mazingira
Mradi unapunguza ukataji wa misitu na kupunguza hewa chafu — mazingira salama zaidi.
Maneno ya REA

Kwa upande wake, Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji wa Mradi kutoka REA, Mha. Emmanuel Yessaya amesema kuwa Wakala ulitenga Fedha kwa ajili ya kufadhili mradi ya usambazaji wa gesi asilia kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini (REF) ambapo takribani kaya 1000 pamoja na taasisi moja zimenufaika kwa kusambaziwa miundombinu ya gesi asilia kwa ajili ya kupikia majumbani katika mkoa wa Lindi na Pwani.

Kauli ya Mha. Emmanuel Yessaya — Kaimu Meneja REA
Mradi huo ni wa kimkakati kwa ajili ya kupunguza gharama za nishati ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kupunguza athari za kimazingira zitokanazo na ukataji wa misitu kwa ajili ya nishati ya kupikia kwa wananchi wanaoishi Vijijini na kwenye vijiji miji.
Maneno ya TPDC

Kwa upande wake Mhandisi wa mradi huo kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Mha. Anthony Karomba, amesema kuwa mradi huo wa kuunganisha wateja wa majumbani kwenye mtandao wa gesi asilia umegharamikiwa kwa fedha nyingi na Serikali kupitia REA na hivyo amewasihi wananchi kuendelea kuilinda miundombinu hiyo.

👷
Mhandisi wa Mradi
Mha. Anthony Karomba (TPDC) aliongooza uunganishaji wa mtandao wa gesi majumbani.
🏠
Walengwa wa Mradi
Kaya ~1,000 na shule 1 katika Kata ya Kisemvule, Mkoa wa Lindi na Pwani.
Faida kwa Wananchi

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa Kata ya Kisemvule wameishukuru Serikali kupitia REA kwa kusambaza miundombinu ya gesi asilia ya kupikia katika miji yao.

1
Kuokoa Gharama za Nishati
Kaya zinazotumia gesi asilia zinapunguza matumizi ya pesa kwa mkaa na kuni kila mwezi.
2
Kulinda Afya za Wananchi
Gesi asilia haizalishi moshi hatari — inaboresha afya hasa kwa wanawake na watoto.
3
Kuongeza Muda wa Kuzalisha Mali
Kupika kwa haraka kunaongeza muda wa shughuli za kiuchumi kwa familia.
4
Kulinda Mazingira
Kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa kunalinda misitu na mazingira ya nchi.
5
Uwezeshaji wa Wanawake
Mradi unawezesha usawa wa kijinsia kwenye shughuli za kiuchumi — Kata ya Kisemvule.

Post a Comment

0 Comments

Post a Comment (0)
3/related/default