By xmation media - Dar es salaam
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, leo Septemba 26, 2025 ameshiriki katika maziko ya marehemu Abbas Ali Mwinyi, ambaye ni kaka wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Maziko hayo yamefanyika Mangapwani, Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, ndugu, jamaa na wananchi waliofika kutoa heshima za mwisho.
Marehemu Abbas Ali Mwinyi atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika familia na jamii.


